Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema inakusudia kuimarisha sekta ya utalii kwa kuweka mawakala  wao katika nchi za nje ili kufanyakazi ya kuitangaza  Zanzibar  katika  nchi  mbalimbali  ili kuwavuta watalii    kujanchini.
Akizungumza  na Mwandishi wetu Afisa Masoko na utangazaji Kamisheni ya Utalii Zanzibar Halfani  Ali Mohammed amesema  ili   kuukuza   utalii   Zanzibar lazima   serikali itekeleze   azma yake ya kuweka wakala katika nchi mbalimbali duniani kutangaza vivutio vya  utalii viliopo nchini.
Hata hivyo amesema    mbali na  kuwepo kwa kituo cha cha wakala katika nchi  ya India kinachotangaza utalii wa Zanzibar  lakini pia serikali imekusudia  kufungua  vituo vyengine vipya  katika nchi ya  China, Israel na Urusi ili kuendelea kutangaza utalii wa Zanzibar.
Aidha  amesema  katika  hatua  hizo zinazotarajiwa kuchukuliwa   ametoa wito kwa wakaazi wa zanziabr  kutunza na kuhifadhi  maeneo  ya vivutio  vya utalii vilivyopo  nchini  pamoja na kuendelea  kudumisha  amani na utulivu.

Zaidi ya watalii  Laki tatu sabini na sita Elfu  mia mbili  arobaini na mbili walitembelea Zanzibar kwa mwaka  2016 huku wageni kutoka nchi za Ujerumani, Italy, Marekani na Israel wanaongoza kuitembelea Zanzibar.
 
Top