Image result for faru mzee zaidi duniani

Tanzania licha ya kuwa na vivutio vingi vya utalii, lakini pia inajivunia kuwa na faru mweusi jike ambae ndie faru mzee zaidi duniani.
Faru huyo maarufu kwa jina la Fausta hivi sasa amehifadhiwa katika eneo maalumu baada ya afya yake kudhoofika. Aboubakar Famau hivi karibuni alikuwa katika hifadhi ya taifa ya Ngorongoro na kutuandalia taarifa ifuatayo.

FARU Fausta ndio anayesadikiwa kuwa na umri mkubwa kuliko Faru wote duniani, mwaka huu amefikisha umri wa miaka 54.
Faru Fausta yupo katika mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, lakini kutokana na uzee wake huo, sasa anakabiliwa na tatizo la macho la kutoona vizuri.
Kufuatia hatua hiyo,uongozi wa Ngorongoro sasa umemuweka katika makazi maalum ndani ya hifadhi hiyo.


Hatua ya mamlaka kuchukua hatua ya kumpa ulinzi maalum Faru Fausta inahofia kushambuliwa na wanyama wengine wakali na hususani Fisi na Simba.


 
Top