Sieny ni eneo lililopo katika Kijiji cha Ngira, Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro, Kaskazini mwa Tanzania, ni miongoni mwa maeneo yanayoheshimika kutokana na imani ya kabila la Wachaga (wamachame) waishio katika eneo hilo.

Ni katika eneo hilo, ndio kunapatikana Daraja la Mungu ambalo wakazi wake wanaamini limejengwa na Mungu, lakini pia kuna mapango yanayotumika kwa matambiko. 
Miaka ya nyuma ya 1979 eneo hili lilikuwa maarufu sana kwa wakazi wa Kijiji  cha Ngira na jirani (Sonu, Uswaa, Mudio na Masama) walikuwa wanakwenda kuabudu na kufanya matambiko mbalimbali wakiamini lolote linajibiwa na Mungu hata kuomba mvua na kupona magonjwa mbalimbali. 
 
Top