Mpanda milima mashuhuri Duniani kwa kutumia Baiskeli ,Juanito Oiarzabal ameweka rekodi ya kuwa Mhispania wa kwanza kupanda Mlima Kilimanjaro huku akitumia saa 31 akiendesha baiskeli katika siku tano hadi kufika kilele cha Uhuru.
Juanito na wenzake wawili , Eduardo Pascuaz na Ramon Abecia waliianza safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli kupitia lango la Kilema.


Juanito Oiarzabal ambaye amepata ulemavu wa kukatika vidole kutokana na barafu katika Milima mbalimbali aliyopanda amesema changamoto aliyokutana nayo wakati wa kupanda mlima ni kuzoea hali ya hewa yamlima ambayo imekuwa ikibadilika kila mara.
 
Top